August 16, 2014


VAN GAAL (KULIA) AKIWA NA KOCHA WA ZAMANI WA MAN UNITED, ALEX FERGUSON.

Saa chache baada ya Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger kusema kikosi chake hakijawa tayari kwa ajili ya Ligi Kuu England inayoanza leo, Louis van Gaal, naye ameonya.
Man United inaanza msimu wa Premier League leo katika mechi dhidi ya Swansea ambayo itapigwa saa 8:45 kwa saa za Bongo.

Van Gaal amesema kikosi chake cha Manchester United hakijaiva vizuri kama anavyotaka huku akitaja sababu kadhaa.
Moja ya sababu alizotoa van Gaal ni kuhusiana na mabadiliko makubwa ndani ya kikosi chake.
Pili akasema kuna baadhi ya wachezaji waliowataka wakawakosa, hivyo wanajipanga na walionao.
Tatu ni kuhusiana na kubadili kwa mfumo anaotaka wautimie wa 3-4-1-2 ambao anasema lazima utawasumbua wachezaji mwanzoni.
Van Gaal amesem mfumo huo utawasumbua wachezaji kutokana na mabadiliko ya makocha watatu ndani ya miezi zita had inane ikiwa ni baada ya kuondoka kwa Alex Ferguson, akatua David Moyes na sasa yeye.
Tayari suala hilo amelifikisha kwa familia ya Glazer ambao ndiyo wamiliki wa Man United na bosi mkubwa Ed Woodward na kuwataka wawe na subira kwa kuwa huenda mwanzo wa Man U unaweza usiwe mzuri sana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic