August 16, 2014




Na Saleh Ally
BURUDANI ya Ligi Kuu England inajuliakana, hata kama msimu utaisha, lakini unaacha gumzo na rekodi kibao zitakazosimuliwa milele.
Premier League au Premiership inaanza leo, utamu wake unajulikana lakini machungu yake pia.
Msimu uliopita ulikuwa na burudani nyingi ambazo zinaweza kupangika kwa namba na kuwa kiburudisho kwa mashabiki kujipungusha kabla msimu wa 2014-15 kushika kasi.
Watanzania wengi kama ilivyo sehemu nyingi duniani watakuwa wanaisubiri ligi hiyo kwa hamu kubwa wakijua kutaandikwa rekodi nyingine tokea itakapoanza hadi inavyosonga mbele.
Lakini si vizuri kuacha burudani ya rekodi au matukio ya kuvutia yaliyojitokeza katika msimu wa 2013-14 ambao ulikuwa una burudani za kila aina.
Kulikuwa na kila aina ya burudani ambayo ilichangia kuandikwa kwa rekodi mpya kibao ambazo pamoja na kuanza kwa msimu mpya, mpenda soka yoyote angependa kuzisoma.
Kupitia namba lakini si kwa kufuata moja hadi mia, badala yake kwa kuchanganya, soka burudani hizo kupitia namba, rekodi ambazo ziliwekwa huku wachezaji wakiwa hawajui kuwa wanaziweka, badala yake kila mmoja alipambana kuipa timu yake ushindi.

0
Hakuna hata timu moja ilimaliza msimu bila ya kupoteza hata mechi moja kama ilivyofanya Arsenal katika msimu wa 1988-89.
1
*likuwa ni mara ya kwanza mabingwa kumaliza nje ya sita bora tokea msimu wa 1994-95 wakati Blackburn Rovers, wakiwa mabingwa wakamaliza katika nafasi ya saba.
*Huu umekuwa msimu wa kwanza wa Premier League, timu mbili kufunga mabao zaidi ya 100. Manchester City ilifunga 102, Liverpool wakapachika 101). Msimu wa 2009-10, Chelsea ilikuwa timu pekee iliyofikisha zaidi ya mabao 100, ilifunga 103.
*Wakati Adam Johnson alikuwa Mwingereza pekee aliyefunga hat trick, Marouane Fellaini alitoa pasi moja tu iliyozaa bao, haladu hakufunga hata moja baada ya kumaliza msimu wa 2012-13 akiwa ametoa pasi tano za mabao na kufunga 11!
2
Timu mbili za Liverpool na Fulham, ndiyo zilimaliza msimu bila ya kucheza hata mechi moja na kupata sare ya 0-0.
4
Beki wa Liverpool, Martin Skrtel ameweka rekodi mpya ya Premiership kwa kujifunga mabao manne katika msimu mmoja tu.
6
Sunderland na Liverpool ndiyo timu pekee zilizojifunga mabao sita kila moja.
7
*Bingwa wa Premier League alipatikana katika mechi ya mwisho kwa mara ya saba katika misimu 22 mfululizo.
* Sunderland ndiyo iliongoza kwa kadi nyingi nyekundu baada ya kupata saba.
*Man United ilipoteza mechi saba za nyumbani, haijawahi kutokea tokea msimu wa 1973-74, halafu ikamaliza ya saba.
8
Daniel Sturridge alikuwa mchezaji wa kwanza wa Liverpool kufunga mabao katika mechi nane mfululizo.
10
*Steven Gerrard alimaliza msimu akiwa na mabao 10, yote ya mikwaju ya penalti.
*Huu ni msimu wa kwanza kuona makocha 10 katika timu 20 za Premier League wakiachana na timu zao.
12
Liverpool ilipata penalti 12 ambazo ni nyingi zaidi kuliko za timu nyingine.

13
Manchester City walifunga mabao 13 kupitia kona wakiongoza kuzidi timu nyingine.
18
 Mfungaji kinda zaidi kwenye Premier League msimu huu alikuwa ni kinda wa Arsenal, Serge Gnabry aliyefunga bao dhidi ya Swansea akiwa na umri wa miaka 18 na siku 76.
25
Timu zilibadilishana kukaa kileleni mwa Premier League katika msimu uliopita.
27
Liverpool ndiyo timu iliyoongoza kwa mashuti ya wachezaji wake kugonga mwaka wa juu maarufu kama ‘mtambaa wa panya’. Iligongesha mara 27.
31
Luis Suarez aliyefunga mabao 31, amekuwa mchezaji wa pili kwenye Premier League kufikisha mabao 30 bila ya mkwaju wa penalti. Wa kwanza alikuwa ni Andy Cole aliyefanya hivyo katika msimu wa 1993-94 kwa kupachika mabao 34.
32
Romelu Lukaku ameweka rekodi ya kufunga mabao 32 kwa misimu miwili akiwa mchezaji aliye kwenye mkopo.
35
Frank Lampard ndiye mchezaji mzee zaidi aliyefunga bao katika msimu uliopita. Akiwa na umri wa miaka 35 na siku 289, alifunga bao dhidi ya Stoke, hiyo ilikuwa Aprili.
59
pamoja na kutimuliwa, Tim Sherwood ameondoka na rekodi kubwa ya wastani wa ushindi ya 59% ambayo ni ya juu kuliko ya kocha mwingine yoyotr aliyewahi kuifundisha Tottenham Hotspur kwenye ligi hiyo.
78
Kocha José Mourinho alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kama kocha wa Chelsea katika mechi mechi yake ya 78 katika Uwanja wa Stamford Bridge.
85
Fulham imeshikanafasi ya pili kuwa timu iliyofungwa mabao mengi zaidi katika mechi 38 za msimu. Ilipachikwa mabao 85, wanaongoza Derby County ambayo walifungwa 89 katika msimu wa 2007-08.
89
Liverpool ndiyo timu iliyofanya mabadiliko machache zaidi kuliko timu nyingine kwenye Premiership msimu huu, ilibadilisha wachezaji mara 89 tu, wakati Chelsea iliongoza kwa kubadili mara 113.
121
Cheick Tiote alipiga pasi 121 wakati Newcastle ikiivaa Crystal Palace na kumfanya awe mchezaji aliyepiga pasi nyingi zaidi zilizofika katika mechi moja kwa msimu wa 2013-14.
999
pamoja na kumaliza katika nafasi ya saba, Manchester United ilishika nafasi ya kwanza kwa kupiga krosi nyingi, ilipiga 999 ambazo ni nyingi kuliko zilizopigwa na timu nyingine yoyote.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic