Unaweza kusema kweli amerejea Premier League, Cesc Fabregas ameshiriki
kuzalisha mabao yote matatu wakati Chelsea ilipoitwanga Burnley kwa mabao 3-1
katika mechi yake ya kwanza ya ligi hiyo, usiku wa kuamkia leo.
Fabregas aliyewahi kukipiga Arsenal na baadaye kwenda Barcelona
alikoanzia, sasa amerejea katika ligi akiwa na Chelsea.
Bao la kwanza lilifungwa na Diego Costa baada ya yeye kupiga shuti
likamgonga beki na kumkuta mfungaji.
Bao la pili lilifungwa na Andre Shurrle baada ya pasi yake tamu na
limepewa kuwa bao la wiki.
Halafu bao la tatu likafungwa na beki Branislav Ivanovic akimalizia
mkwaju wa kona wa Fabregas.
0 COMMENTS:
Post a Comment