Gazeti maarufu la michezo la AS la nchini
Hispania, limetumia ukurasa mzima kuelezea ziara ya kikosi cha wakongwe cha
Real Madrid.
Madrid watacheza mechi ya kirafiki dhidi ya
Tanzania Eleven ambao wameanza kujifua chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa.
Mechi hiyo itapigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Madrid wanatarajia kuanza kuwasili kesho.
Kati ya wadhamini wa ziara hiyo na mechi ya kirafiki ni TSN ambao pia ni waratibu wa ziara hiyo, Hoteli ya Sapphire, Bin Slum, Gazeti la Championi na kampuni ya ndege ya Fast Jet.
0 COMMENTS:
Post a Comment