Pamoja
na kuonekana Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri ni mtaratibu, lakini nidhamu
katika kikosi cha Simba imeimarika zaidi.
Mazoezi
wamekuwa wakifanya kwa juhudi kubwa na kutekeleza yale wanayoelekezwa na kocha
wao huyo raia wa Zambia anayesaidiwa na Selemani Matola.
Phiri
ni mtaratibu, lakini mara kadhaa amekuwa akiwabadilikia wachezaji wanaoonekana
kutokuwa makini.
Awali
wachambuzi walieleza kwamba wachezaji wanahitaji mtu ‘mkatili’ au mkorofi kama
Zdravko Logarusic aliyetimuliwa.
Lakini
inaonekana aina ya kocha kama Phiri atakuwa mfano mzuri kwa kuwa wachezaji ni
lahisi kumwelewa na wanatekeleza anayowaelekeza.
0 COMMENTS:
Post a Comment