Kocha
Zdravko Logarusic amesema bado hajafanikiwa kupata ajira mpya.
Loga
ameiambia SALEHJEMBE kutoka kwao Croatia, baada ya kufutwa kazi na Simba, sasa
anaendelea na mapumziko huku akisubiri ajira mpya.
“Nitaendelea
kutafuta na pia kusubiri kama kuna timu zitakuwa zinanihitaji.
“Lakini
sasa bado kidogo, hakuna timu wala sina ajira mpya,” alisema Loga akifafanua
taarifa za kwamba Gor Mahia ya Kenya imeanza mazungumzo naye.
Loga
aliifundisha Simba kwa nusu msimu, lakini baada ya kuingia mkataba mpya wa
mwaka mmoja, hakupata nafasi ya kuendelea kuitumikia.
0 COMMENTS:
Post a Comment