August 24, 2014



Mohamed Abdallah, Zanzibar
Andrey Coutinho amefanikiwa kupiga bao na kuisaidia Yanga kuifunga Shangani inayoshiriki Ligi Daraja la Pili hapa.

Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, moja likiwa limesababishwa na Salum Telela ambaye alipiga krosi safi mabeki wa Shangani wakajifunga.
Mechi hiyo kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa, ilikuwa nzuri nay a kuvutia.
Coutinho alionekana kuwa fiti zaidi huku Mbrazili mwenzake, Jaja akibanwa.
Yanga ilicheza kwa kuelewana tokea mwanzo, lakini baadaye Shangani nao walijibu mashambulizi na kuifanya mechi kuwa ya ushindani.
Chini ya Marcio Maximo, Yanga itacheza mechi nyingine moja ya kirafiki Jumatano kabla ya kurejea jijini Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic