FIGO |
Mshambuliaji nyota wa zamani wa Real Madrid, Luis
Figo amethibitisha kwa mdomo wake kwamba anakuja nchini.
Katika mahojiano kupitia simu, Figo amezungumza na
Saleh Ally na kusema anakuja nchini kesho kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya
Tanzania Eleven kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi.
Lakini akasisitiza, asingependa kuondoka nchini
hadi atakapouna Mlima Kilimanjaro.
“Ninafurahi kuja Afrika kucheza, najua kitakuwa
kitu kipya na kizuri sana katika maisha ya soka.
“Lakini najua kuhusiana na Mlima Kilimanjaro,
nisingependa kuondoka bila ya kuuona Mlima Kilimanjaro.
“Waambie watu waje tufurahie pamoja na Real Madrid
imeonyesha inaijali Afrika na Tanzania ndiyo watakuwa wenyeji wetu.”
Hii ni mara ya kwanza Figo kufanya mahojiano moja
kwa moja na chombo cha habari.
Figo anawasili nchini kesho usiku akiongozana na
kiungo Christian Karembeu raia wa Ufaransa ambaye asili yake ni bara la Afrika.
Mechi hiyo ya Jumamosi, tayari imekuwa gumzo na
tiketi zimeshaanza kuuzwa katika vituo mbalimbali vya mafuta vya TSN na maduka
ya Supermarket za TSN.
0 COMMENTS:
Post a Comment