FIGO AKIWA NA SALEH ALLY. |
Na Saleh Ally
KWA Hispania wanaamini Gareth Bale ndiye
mrithi mpya wa winga au kiungo wa pembeni matat, Luis Figo ambaye wakati wa
enzi zake anajulikana.
Sifa kubwa ya Figo ni kasi, krosi za ‘moto’
lakini mashuti ambayo yanaelekezwa langoni wakati akiwa katika kasi kubwa.
Figo alitua Madrid mwaka 2000 akitokea
Barcelona, aliichezea hadi 2005 akibeba makombe lukuki. Ubingwa wa La Liga mara
mbili (2000-01, 2002-2003), Super Cup Hispania (2001 na 2003).
SALEH ALLY AKIZUNGUMZA NA RAYCO GARCIA, KULIA NI KAREMBEU NA KATIKATI YAO NI SANZ. |
Achana na makombe hayo lakini Ligiya
Mabingwa Ulaya mwaka 2002 ambao pia walibeba Uefa Super Cup kama ambayo Madrid
wameibeba kwa mara nyingine.
Hiyo ni Madrid lakini alibeba makombwe
mengine ya La Liga, Copa del Rey, Super Cup ya Hispania na ile ya Uefa akiwa na
Barcelona.
Figo pamoja na kutoa pasi tamu za mwisho maarufu kama asisti,
pia ana uwezo wa kucheka na nyavu kwa kuwa akiwa na Madrid alicheza mechi 164
alipachika mabao 36 akionyesha ni moto kwa kuwa Barcelona alicheza mechi 172
akapiga mabao 30.
Figo leo atakuwa kwenye kikosi cha wakongwe
wa Real Madrid ambao wametua nchini tayari kuwavaa Tanzania Eleven ambao wako
fiti kweli na tayari kwa kuonyeshana kazi.
Katika mahojiano mafupi na SALEHJEMBE, Figo
mwenye miaka 41 sasa, anasisitiza hawezi kukimbia kama zamani, lakini uwezo
wake ni burudani tosha.
“Hauwezi kupingana na umri, lakini aina
yangu ya uchezaji inabaki ileile. Vizuri zaidi nacheza na watu wanaonijua au
tunajuana vizuri,” anasema huku akitabasamu.
“Njoo siku ya mechi uone, ninaweza kufanya
kila unachokijua, kukimbia, pasi nzuri, kufunga na mengine na ndiyo wanavyoweza
kufanya wengi katika kikosi chetu.
“Wengi umri umekwenda, lakini wanacheza soka
la kuvutia,” anasema Figo ambaye aliichezea timu ya taifa ya Ureno mechi 127 na
kufunga mabao 32. Kwenye Kombe la Dunia mwaka 2006 ndiye alikuwa nahodha wa
timu hiyo.
Leo Figo atakuwa kazini kupambana na mabeki
wa Tanzania Eleven akiwemo Abubakari Kombo na Shadrack Nsajigwa ambao wana sifa
ya wachezaji wa kimataifa wa kiwango cha juu kwa ‘levo’ ya kwetu.
Inaonekana itakuwa burudani nzuri lakini kwa
muonekano, Figo ni mchezaji ambaye anafanya mazoezi ya kutosha.
“Mazoezi kwangu si kwa sababu ya mechi,
nafanya hivyo kama sehemu ya maisha yangu, nina diet maalum kila baada ya
kipindi fulani.
“Suala la kuwa niko fiti au la, lisikupe
hofu. Kikubwa nasisitiza njoo utuone (Real Madrid), nina uhakika utafurahi,
halafu utaniuliza zaidi,” analihakikishia Championi.
Kwa tuzo binafsi alizowahi kupata
zinathibitisha kuwa Figo ni kati ya wachezaji wa kiwango cha juu kabisa
waliowahi kutokea Ureno na duniani kote.
Kupitia makubwa aliyoyafanya akiwa na
Barcelona, Madrid na timu ya taifa ya Ureno inamfanya awe ndiye mchezaji
maarufu zaidi katika klabu hizo maarufu za Hispania.
Alikuwa nyota na gumzo ndani ya Barcelona
kuanzia mwaka 1995 hadi 2000, akaondoka na kujiunga na Madrid mwaka 2000, wengi
wakidhani kasi ingepungua. Lakini miaka mingine aliendelea kuwa moto na gumzo
katika jiji la Madrid.
Amewahi kutwaa tuzo binafsi kama zile za Mchezaji
bora wa Ulaya chini ya miaka 21 (1991), Mfungaji bora wa Hispania (1994),
Mchezaji bora wa Ureno (1995, 1996, 1997, 1998, 1999, 2000).
Mchezaji
bora wa kigeni wa Hispania (1999, 2000 na 2001), Mchezaji Bora wa
Ulaya (2000), Mchezaji bora wa Dunia (2001), pia ni mmoja wa wachezaji bora 100
wa karne walioteuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Awali alisema ni lazima auone Mlima wa
Kilimanjaro ambao ni mrefu kuliko yote Afrika. Kweli hilo litakamilika baada ya
kampuni ya TSN kupanga ratiba ya kuwapeleka.
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TSN, Farough
Baghoza, amesema kesho ndiyo itakuwa safari ya kwenda Mlima Kilimanjaro.
“Lengo ni kama kutembelea na kuangalia
utajiri wa Tanzania. Kupanda haitawezekana kutokana na ratiba zao kuwabana na
unajua inachukua muda kuupanda mlima huo,” anasema Farouk.
Mechi ya leo, tayari imekuwa gumzo katika
viunga vya jiji la Dar es Salaam na kuna taarifa baadhi ya wadau kutoka nchi
jirani za Kenya na Uganda, wameanza kuwasili nchini kuhakikisha wanaishuhudia
mechi hiyo.
Mchezaji bora wa Ulaya chini ya miaka 21
(1991), Mfungaji bora wa Hispania (1994), Mchezaji bora wa Ureno (1995, 1996, 1997, 1998, 1999,
2000).
Mchezaji
bora wa kigeni wa Hispania ( 1999,2000 na 2001), Mchezaji Bora wa
Ulaya (2000), Mchezaji bora wa Dunia (2001), pia ni mmoja wa wachezaji bora 100
wa karne walioteuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Fin.
0 COMMENTS:
Post a Comment