Gumzo la kipigo cha mabao 2-1 ilichokipata Man
United kutoka kwa Swansea kimelifunika jiji la Dar es Salaam.
Gumzo hilo limefanya mashabiki wa Yanga na
Simba, kuzisahau kwa muda timu zao za nyumbani na zaidi kujadili kuhusiana na
Man United.
Uchunguzi wa SALEHJEMBE unaonyesha watu wengi
wamejadili kuanzia jioni Man United ilipochapwa kwenye mechi ya lipi.
Kwenye email ya blogu hii, mashabiki 1600
walituma ujumbe kulaumu kipigo hicho.
Wengine 2116 walituma ujumbe kwenye akauni ya
Facebook ya SALEHJEMBE, wakilalama, wengine wakiunga mkono au kumbeza Kocha
Luis van Gaal na wachezaji wake.
Asilimia 16 hadi 20 zilizotumwa zilimuunga
mkono au kumkumbushia kocha aliyeyetimuliwa, David Moyes.
Kipigo hicho katika mechi ya ufunguzi ya ligi
kimekuwa cha kwanza kwa Man United tokea ilipofungwa mwaka 1972.
0 COMMENTS:
Post a Comment