Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri ameamua kikosi chake kuanza mazoezi
mara mbili kwa siku.
Leo Simba ikiwa kambini mjini Zanzibar ilifanya mazoezi mara moja tu
kwenye ufukwe wa bahati ya Hindi.
Lakini taarifa zimesema kuwa Phiri ameamua sasa kikosi hicho kufanya
mazoezi mara mbili kwa wiki.
“Kweli Kocha Phiri amesema kuanzia kesho Jumatatu, mazoezi yatakuwa ni
asubuhi na jioni.
“Halafu amesisitiza suala la mechi za kirafiki kwa ajili ya kukiona
kikosi,”zilieleza taarifa kutoka kambini Simba.
Phiri amerejea kuinoa Simba baada ya kutimuliwa kwa Zdravko Logarusic.
0 COMMENTS:
Post a Comment