Manchester
United inajiaandaa kuhakikisha inatenga kitita lundo cha hadi pauni milioni 100
kuhakikisha inamnsa kiungo wa pembeni mwenye kasi kutoka Real Madrid.
Angel di
Maria ndiye chaguo la Kocha Louis van Gaal ambaye ameuambia uongozi wa Man
United kwamba ufanye kila linalowezekana ili Di Maria atue OT.
Van Gaal
amezungumza na bosi mkubwa wa Man United, Ed Woodward na kumuambia azungumze na
Madrid kuhusiana na Muargentina huyo.
Iwapo itafanikiwa
kumpata, United italazimika kulipa mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki. Fedha ambazo
wanalipwa nyota wa kikosi hicho kama Wayne Rooney na Robin van Persie.
Tayari United
imeanza ligi kwa kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Swansea hivyo kufanya van Gaal
aanze kuangalia urekebishaji wa makosa yaliyojitokeza.
0 COMMENTS:
Post a Comment