SIWA (KULIA), WAKATI AKIWA YANGA PAMOJA NA MENEJA WAKE, HAFIDH SALEH NA FRED FELIX MINZIRO. |
Aliyekuwa kocha wa makipa wa timu ya Yanga, Razack Siwa, hatimaye
ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu ya Coastal Union ya Tanga.
Coastal Union inajiandaa na maandalizi ya msimu ujao wa Ligi Kuu
Tanzania Bara utakaoanza mwezi ujao.
Siwa ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu hiyo kwa kipindi
cha mwaka mmoja, lengo likiwa kuipa mafanikio makubwa timu hiyo msimu ujao.
Tayari Siwa ameungana na wachezaji wa timu hiyo leo kupanda ndege
kuelekea visiwani Pemba ambako timu hiyo inakwenda kuweka kambi ikijiwinda na
michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Akizungumza kabla ya timu hiyo kuondoka, Katibu Mkuu wa Coastal
Union, Kassim El Siagi, amesema kuwa kocha huyo wa makipa anachukua nafasi
iliyokuwa wazi kutokana na kutokuwa na mwalimu maalumu wa kuwafundisha walinda
mlango wa Coastal Union.
0 COMMENTS:
Post a Comment