MAXIMO KAZINI. |
Na Mohammed Selemani, Pemba
Kocha wa Yanga, Mbrazili Marcio Maximo, juzi alikuwa mkali kwa
wachezaji wake ambao walikuwa wakizembea mazoezini.
Yanga ipo hapa kisiwani Pemba kwa ajili ya kujiandaa na Ligi Kuu
ya Tanzania Bara pamoja na mchezo wa Ngao ya Jamii utakaopigwa baadaye mwezi
ujao.
Kocha huyo ambaye alionekana kuwa mkali mara kwa mara, alianza kwa
kuwakimbiza wachezaji wake kwa zaidi ya dakika 20 na baadaye kunyoosha viungo
kabla hawajaanza kuchezea mpira.
Maximo alionekana kuwa mkali kila mchezaji wake alipokuwa
akipoteza mpira kizembe ambapo alimwita na kuongea naye kwa ukali.
Timu hiyo inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki kesho ambao
utakuwa wa kwanza kwa wachezaji wapya wa timu hiyo kuonekana wakiwa uwanjani
wanakipiga.
0 COMMENTS:
Post a Comment