Hatimaye
Bodi ya Ligi (PLB) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wameachia ratiba ya
Ligi Kuu Bara msimu wa 2014-14.
Kinachovutia
zaidi ni kwamba, watani Yanga na Simba watakutana ‘asubuhiii’, yaani ikiwa ni
baada ya kila timu kucheza mechi tatu tu za ligi.
Dar
es Salaam derby imepangwa Oktoba 12, ikiwa ni kila baada ya timu kucheza mechi
tatu tu.
Kawaida
Yanga na Simba hukutana mwishoni mwa mzunguko wa kwanza na ule wa lala salama. Sasa
mambo mapema kabisa.
Kabla
ya mechi hiyo, Yanga itafungua dimba na Mtibwa Sugar mjini Morogoro wakati
Simba itakuwa Dar es Salaam kuwakaribisha Wagosi wa Kaya, Coastal Union.
0 COMMENTS:
Post a Comment