Sasa uhakika Luis Nani anarudi kwao Ureno kuichezea
Sporting Lisbon ambayo ilimkuza kisoka.
Manchester United imefikia makubaliano dili la pauni
milioni 16 na Wareno hao kumnasa beki Marcos Rojo raia wa Argentina
Rojo, alishasema ni ndoto yake kujiunga na United na
sasa anajiunga nayo. Ila United itaendelea kulipa mshahara wa Nani hadi mwisho
wa mkataba.
Rojo mwenye miaka 24 anakuwa kati ya wachezaji
walioingia kwenye listi ya United baada ya kuanza Ligi Kuu England kwa kipigo
cha mabao 2-1 kutoka kwa Swansea.
0 COMMENTS:
Post a Comment