September 17, 2014

KALI ALIYEWAHI KUICHEZEA YANGA AKISALIMIANA NA KOCHA WA YANGA, MARCIO MAXIMO WAKATI WA MECHI YA NGAO YA JAMII, JUMAPILI ILIYOPITA.

Kocha Msaidizi wa Azam FC, Kali Ongala, ameukubali uwezo wa Mbrazili, Geilson Santos Santana ‘Jaja’ wa Yanga na akasema wazi kuwa wanaompinga wanamuonea na hawajui uzuri wa mchezaji kama huyo kikosini.

Kauli ya kocha huyo inakuja baada ya kuwepo kwa maneno mbalimbali kuhusu straika huyo aliyetupia mabao mawili juzi na kuisaidia Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Azam kuwa si chaguo sahihi kwa Yanga kwa ajili ya msimu ujao kutokana na staili ya uchezaji wake.

Ongala aliyewahi kuwa mshambuliaji hatari wa Abajalo ya Sinza na Yanga alifafanua kuwa Watanzania walio wengi wanapenda wachezaji wenye spidi na chenga nyingi kama Mrisho Ngassa na hawapendi kumuona mchezaji mwenye kutulia uwanjani na kufanya kilichomleta, ndiyo maana hawaelewi umuhimu wa wachezaji kama Jaja wanapokuwa uwanjani.

“Wengi wanapenda mchezaji mwenye spidi na vyenga vingi kama Mrisho Ngassa, sasa si kila mchezaji yupo hivyo, kwa sababu kila mtu ana silaha yake aliyojaaliwa nayo kwenye soka. Jaja ni straika na kazi yake iliyomleta uwanjani ni kufunga, hayo mambo mengine watafanya wengine.

“Kwangu mimi Jaja ni mchezaji mzuri na anayeijua kazi yake na ana msaada kwa timu kwa sababu anafanya kitu muhimu zaidi katika matokeo ya mechi. Mimi nawashangaa sana wanaomlaumu eti hajui mpira au hana msaada kwa timu kutokana na staili yake ya uchezaji.
“Wanashindwa kuelewa na kujua umuhimu wake, ndiyo maana wanamlaumu pasipo sababu ya maana, nafikiri wangetulia tu ili Jaja afanye kazi yake ya kufunga pekee anayoifahamu na kuipa faida timu.”

Jaja amesajiliwa Yanga hivi karibuni kwa mkataba wa miaka miwili na tayari amefanikiwa kufunga mabao matano ndani ya mechi tano alizoichezea timu hiyo, zikiwamo nne za kirafiki na moja dhidi ya Azam wikiendi iliyopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic