September 22, 2014


Aliyewahi kuwa Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni, amesema mshambuliaji wa kimataifa wa Simba, raia wa Uganda, Emmanuel Okwi, anateswa na mzimu wa marehemu, Patrick Mafisango kwa kuwa ndiye aliyekuwa akimchezesha.

Okwi amesajiliwa na Simba katika dakika za mwisho lakini alikuwa hajaonyesha ubora wake kwenye mechi za kirafiki alizocheza kabla ya jana kuivaa Coastal.

Kibadeni amesema Okwi anahitaji ajipange ipasavyo ili aweze kupata nafasi ya kucheza Simba na kumpata mtu wa kumchezesha kama ilivyokuwa kwa Mafisango ambaye ndiye aliyekuwa msaada mkubwa kwake.
“Okwi ninayemjua mimi si huyu wa sasa kwani kiwango chake kimeshuka mno, hivyo anahitaji kujipanga ipasavyo kwa kuonyesha juhudi za hali ya juu ili aweze kupata nafasi katika kikosi cha kwanza.
“Zamani wakati anaichezea timu hiyo alikuwa na mtu wa kumchezesha, marehemu Mafisango, hivyo kwa sasa anahitaji mtu mwingine aweze kumchezesha na kuwa katika kiwango kizuri kama cha awali,” alisema Kibadeni.





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic