September 22, 2014


Kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohammed, amesema alitumia karibu wiki nzima kuyasoma mabao ya straika wa Yanga, Geilson Santos ‘Jaja’ ili amzuie asilete madhara langoni mwake.


Mbinu hiyo ya Mohammed ambaye aliwahi kuichezea Yanga, ilizaa matunda kwani aliokoa penalti ya Mbrazili huyo pamoja na michomo mingine hatari katika mchezo wa Ligi Kuu Bara baina ya timu hizo, juzi kwenye Uwanja wa Jamhuri, Moro.

Mohammed alishtushwa na uwezo wa Jaja mara baada ya kumtungua kipa wa Azam FC, Mwadin Ally kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii wiki moja iliyopita, ndiyo akaamua kumfungia kazi.

Kipa huyo ambaye inaaminika ndiye alikuwa nyota wa mchezo wa juzi, alisema: “Ukweli hilo liliniongezea umakini kama ulivyoona nilivyokuwa nikimchukulia mipira eneo la hatari.”


Mohammed pia amewahi kuichezea Majimaji ya Songea ambayo hivi sasa inashiriki Ligi Daraja la Kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic