September 22, 2014


Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, amewataka mashabiki wa timu hiyo kutokatishwa tamaa na matokeo ya mchezo wa juzi Jumamosi wa ligi kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri, mjini hapa na timu yake kupokea kipigo cha mabao 2-0.


Akizungumza baada ya mchezo huo, Maximo alisema mechi hiyo ilikuwa ngumu na wachezaji wake walipambana hadi dakika ya mwisho lakini bahati haikuwa yao.

Maximo alisema sasa anajipanga upya kuelekea mchezo ujao na anaamini Yanga itafanya vizuri katika ligi hiyo.
“Mpira ndivyo ulivyo, siku nyingine inakuwa ndiyo na wakati mwingine inakuwa hapana,” alisema.

Hata hivyo, kocha huyo alilalamikia hali ya Uwanja wa Jamhuri kuwa si nzuri na iliharibu mipango mingi ya wachezaji wake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic