September 22, 2014



Mapenzi kwa Chelsea yameshindikana kufichika kwa kiungo Frank Lampard, kwani alitaka kumwaga chozi.
Lampard amekiri kwamba alishindwa kujizuia na ilikuwa nusura amwage chozi baada ya kuifungia Man City bao la kusawazisha dhidi ya Chelsea akiwa anatokea benchi.

“Kweli nilijisikia vibaya lakini mimi ni mchezaji wa kulipwa, ninatakiwa kuonyesha hilo.

“Ilikuwa ni lazima niingie na mpira wa krosi niliopigwa na Milly ulikuwa bora, ulikuwa ni lazima niutendee haki.
“Nimefurahia kuifungia timu ninayoitumikia, lakini sijafurahia kuifanyia hicho Chelsea.
“Nimekuwa pale kwa misimu 13 yenye mafanikio na mapenzi makubwa kwa mashabiki, lazima nitajisikia vibaya,” alisema Lampard.
Chelsea chini ya bosi Jose Mourinho ilimuuza Lampard Marekani na baadaye akarejea Man City kwa mkopo.

Jana alisawazisha na kufanya matokeo ya mwisho kati ya wenyeji Manchester City waliokuwa pungufu baada ya Zabaleta kulambwa kadi nyekundu na Chelsea kuwa sare ya 1-1.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic