September 17, 2014


Licha ya kushinda mabao 3-0, kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa, amefunguka kuwa, Azam ilicheza vizuri zaidi yao katika mechi ya Ngao ya Jamii, Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa.


Ngassa amesema kuwa Azam walionyesha kiwango kikubwa kipindi cha kwanza na Yanga walicheza kawaida sana.

Aliongeza kuwa, tatizo lililosababisha wasifunge mabao kipindi cha kwanza ilitokana na mshambuliaji wao, Mbrazili, Geilson Santana ‘Jaja’ kutotokea mapema kwenye boksi kwa ajili ya kuunganisha krosi.

“Azam walicheza vizuri sana tofauti na sisi ambao tulikuwa kawaida tu, hasa kipindi cha kwanza kwa kuwa Jaja alikuwa akichelewa kuingia kwenye boksi la penalti la wapinzani lakini tunashukuru tumeshinda bao hizo tatu,” alisema Ngassa na kuongeza:

“Inaniuma kwa kuwa sijafunga bao lolote licha ya kupata nafasi nyingi lakini ilinitokea kwa bahati mbaya.”

Katika mechi hiyo, Yanga ilibanwa sana katika kipindi cha kwanza, lakini Azam FC wakashindwa kuzitumia nafasi walizozipata.
katika kipindi cha pili, ngoma ikabadilika na Yanga kutawala huku wakifanikiwa kupata mabao matatu yaliyoinyamazisha Azam FC.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic