September 17, 2014

KISIGA (KATIKATI)...

Zikiwa bado siku chache ili kuanza kwa michuano ya Ligi Kuu Bara, kiungo mshambuliaji wa Simba, Shabani Kisiga, amewapa somo zito wachezaji wenzake wa timu hiyo, Emmanuel Okwi na Paul Kiongera kwa kuwataka kuachana na utani pindi wanapokuwa uwanjani na badala yake wapambane mwanzo mwisho.

Kisiga ambaye amejiunga na Simba hivi karibuni akitokea Mtibwa Sugar, amesema kuwa, Okwi, Kiongera pamoja na yeye mwenyewe, kwa sasa ndiyo wachezaji wa klabu hiyo wanaotupiwa macho na mashabiki, hivyo wanatakiwa kufanya kazi kikweli.

Kikosi cha Simba kwa misimu miwili mfululizo, kilishindwa kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu na kujikuta kikikosa nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa.
“Tuna kazi kubwa ya kufanya safari hii, hivyo utani hautakiwi kabisa uwanjani, kila mchezaji anatakiwa kupambana kwa nguvu zake zote ili aibu ambayo timu hii imeipata miaka iliyopita isitokee tena.
 “Hata hivyo, wachezaji ambao wanatakiwa kuwa makini zaidi ni wale tuliojiunga na Simba hivi karibuni kwa sababu macho na masikio ya mashabiki wa timu yapo kwetu,” alisema Kisiga.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic