September 22, 2014


Kocha Mkuu wa Prisons ya Mbeya, David Mwamwaja amesema wanataka kuendeleza vipigo kwa lengo la kujiimarisha kileleni.

Mwamwaja aliyewahi kuinoa Simba, amesema ushindi wao wa kwanza wa ligi katika mechi ya kwanza, umewapa nguvu za kutaka kuendelea kujikusantia pointi tatu.
Prisons iliichapa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mabatini Mlandizi, Pwani.
“Mechi ilikuwa ngumu lakini tumefurahia kushinda. Tunataka kushinda zaidi na tumeanza kucheza mechi kadhaa za kirafiki kujiimarisha.
“Tutacheza na Ashanti iliyo daraja la kwanza kama kujiweka sawa zaidi. Halafu tutarudi kwenye ligi kutafuta ushindi zaidi.

“Unaposhinda mapema mapema, unajiweka vizuri na kuepuesha presha mwishoni mwa ligi ambako siku zote kunakuwa pagumu,” aliongeza Mwamwaja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic