September 22, 2014


Kocha wa timu ya OFI ya Ligi Kuu Ugiriki, Gennaro Gatuso ameshindwa kuonyesha uvumilivu kwenye mkutano wa waandishi na kuanza kuporomosha matusi.
Gatuso, kiungo mkorofi wa zamani wa AC Milan, alianza kuporomosha matusi kutokana na kuzidiwa maswali.

Timu yake iko katika nafasi ya nane katika msimamo wa ligi baada ya kushinda mechi mbili, imepoteza mbili na Gatuso amekuwa hana raha.
Gatuso ,36, aliuliza kutokana na mwenendo mbaya wa timu yake ambayo inaelezwa kutokuwa katika hali nzuri ya kiuchumi.
 
GATUSO (KULIA) AKIMPIGA MKWARA HAMSIK WA NAPOLI WAKATI AKICHEZA SERIE A AKIWA NA AC MILAN.
Alisema: “OFI sio Real Madrid, sio Barcelona. Ninataka wachezaji wangu kucheza kwa kujituma, tena kwa moyo.
“Sitaki visingizio eti klabu haina mshahara (tusi)," akiinua kidole cha kati kuonyesha ishara ya tusi kulielekeza upande wa waandishi.

“Kwa waandishi pia mmekuwa mkiandika eti naondoka, naondoka wapi, nani kawaambia, sijaja hapa kwa ajili ya kula raha.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic