September 20, 2014


Na Saleh Ally
LIGI Kuu Bara inaanza leo, hakuna ubishi kati ya binadamu walio kwenye presha ya juu ni makocha wakuu 14 wanaoshiriki ligi hiyo.

Hauwezi ukasema kuna kila kocha atakuwa anataka kombe, wako wanaamini kuwa kuna ugumu lakini kila mmoja atajaribu ili alipate.
Kuna madaraja mawili katika mioyo au malengo ya makocha hao. Kwanza ni kulipata kombe hilo na kushiriki michuano ya kimataifa, hizo ni nafasi mbili, ya kwanza na ile ya pili.
Ikishindikana ni mpango wa pili, kubaki Ligi Kuu Bara ili msimu mwingine waendelee kujaribu kupambana kubeba kombe, kushiriki michuano ya kimataifa au kubaki.
Kwa makocha hao wa timu 14, kivutio ni hivi, kati yao wenyeji ni nane na sita waliobaki ni wageni ambao wanatokea katika nchi tano.
Kenya ina makocha wawili ambao wanazinoa Coastal Union na Ruvu Shooting, halafu wageni wengine wanne ni kutoka Zambia-Patrick Phiri wa Simba, Brazil, Marcio Maximo (Yanga), Cameroon-Patrick Omog (Azam FC) na Uganda-Jackson Mayanja (Kagera).
 Makocha hao sita wa kigeni wanapambana wao kwa wao halafu dhidi ya wenyeji wakati wenyeji wanapambana dhidi ya wageni.
Kombe litachukuliwa na wazalendo wanane au lazima litakwenda nje. Maana makocha wageni wamekuwa wakitawala.
Kuna mwenyeji anaweza kupambana nao, Juma Mwambusi wa Mbeya City alionyesha njia na kushika nafasi ya tatu msimu uliopita. Vipi kuhusu msimu huu?
Kama yeye akishindwa, mwali atakwenda Brazil iwapo watamchukua Yanga, Zambia kama ataenda Simba au atabaki Cameroon kwa Omog ndani ya Azam FC?
Lakini kuna Wakenya wawili na Mganda mmoja ambao pia watakuwa wanapambana. Maswali ni mengi lakini majibu yanaanza leo.


MABOSI 14 LIGI:
Yanga – Marcio Maximo (Brazil)
Ndanda FC- Denis Kitambi (Tanzania)
Polisi Moro- Aldoph Rishard (Tanzania)
Stand United- Emmanuel Masawe (Tanzania)
Mbeya City- Juma Mwambusi (Tanzania)
Azam FC- Joseph Omog (Cameroon)
Simba- Patrick Phiri (Zambia)
JKT Ruvu- Fred Felix Minziro (Tanzania)
Mtibwa Sugar- Mecky Maxime (Tanzania)
Ruvu Shooting- Tom Olaba (Kenya)
Prisons – David Mwamwaja (Tanzania)
Mgambo- Bakari Shime (Tanzania)
Coastal Union- Yusuf Chippo (Kenya)
Kagera Sugar-Jackson Mayanja (Uganda)
FIN.


Viwanja vilivyorejea ligi kuu..
INGAWA zimepanda timu tatu kwenye Ligi Kuu Bara, mbili zikiwa ‘mpya’ kabisa, ni viwanja viwili tu ndiyo vitakuwa vimerejea kwenye ligi hiyo.
Kambarage Shinyanga ambao utatumiwa na

Kagera-Kaitaba
Ndanda-Nangwanda
Stand-Kambarage
Yanga, Simba-Taifa
Mtibwa, Polisi-Jamhuri
Prisons, Mbeya City- Sokoine
Azam FC- Chamazi
JKT Ruvu, Ruvu-Mabatini
Coastal, Mgambo- Mkwakwani


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic