September 20, 2014


Na Mwandishi Wetu
HAKUNA anayeweza kukataa kwamba timu tatu au nne zitakazokuwa na msimu mgumu zaidi kwenye Ligi Kuu Bara, Azam FC na Mbeya City zitaongoza.

Simba inaweza kuwa moja ya timu hizo kwa kuwa inataka kujinyanyua na kurejea kwenye daraja la heshima yake.
Lakini Azam FC na Mbeya City ndiyo wenye kazi ngumu zaidi kwa kuwa msimu wao wa kwanza wa ligi kuu wakamaliza wakiwa katika nafasi ya tatu.
Hakuna timu ambayo itakwenda kucheza dhidi ya Mbeya City ikiwa ‘ime-relax’ kwa kuwa inajua ni kibarua kigumu.
Pia hakuna timu itataka kugeuzwa sehemu ya njia ya mafanikio ya Mbeya City kwa mara ya pili mfululizo.
Wao Mbeya City ambao wanadhaminiwa na kampuni ya Bin Slum Tyres ambayo inatangaza betri zake za RB, imeanza maandalizi ikijua msimu huu utakuwa mgumu kwao.

Timu chini ya Kocha Juma Mwambusi imeanza maandalizi na hadi jana ilikuwa imejichimbia nje ya jiji la Mbeya. Hii inaonyesha kiasi gani wamepania kuendeleza walichokianzisha msimu uliopita.
Deni lao ni kwamba, katika msimu wa kwanza wa ligi kuu. Mbeya City chini ya kocha Mzalendo, Mwambusi ilifanikiwa kufikisha pointi 48, si mchezo.
Kumbuka, Simba iliyoshika nafasi ya nne ilikuwa na pointi 38, tofauti ya pointi 11 dhidi ya Mbeya City.
Kwa hesabu za kawaida, ili Mbeya City ifanikiwa, lazima iwe na uhakika wa kufikisha pointi hizo, halafu na zaidi. Japo wingi au uchache wa pointi, pia unaweza kupunguzwa au kuongezwa kutokana na ugumu au ulaini wa ligi.
Azam FC:
Hawa ndiyo mabingwa waliositisha utawala wa Simba kwa zaidi ya miaka 10. Lakini ndani ya miaka 25 Mtibwa Sugar pekee iliingia katika ya wakongwe Yanga na Simba na kutwaa kombe baada ya Coastal Union mwaka 1988 na baadaye Mtibwa Sugar mara mbili.
Mtibwa Sugar pekee walifanikiwa kutwaa mara mbili mfululizo dhidi ya wakongwe hao. Azam FC wataweza?
Maana wakongwe pia ni wabishi na safari hii wana vikosi imara. Wanataka kurudisha heshima na hawatakuwa tayari kuendelea kulikosa kombe.
Azam FC ilifikisha pointi 62 zilizoiewezesha kutwaa ubingwa msimu uliopita ikiwa ni ongezeko la point inane tu ukilinganisha na msimu wa 2012-13 ambao Yanga ilikuwa bingwa na pointi 60.
Azam FC inaweza kujiongeza, haina kikosi kinachobadilika sana, lakini Yanga katika misimu miwili imekuwa bingwa na nafasi ya pili.
Simba ndiyo ina deni kubwa, misimu yote miwili haijabeba ubingwa na imeshika nafasi ya tatu na nne. Sasa inataka kurudi.
Hii ndiyo picha halisi ya ushindani hata kabla ya kuanza kwa ligi na ukiangalia katika timu hizi nne, Yanga, Simba, Azam FC na Mbeya City, yupi atashika mbili bora.
Je, kati ya Polisi Moro, Stand United na Ndanda FC, kati yao kuna mgeni ataingia kati kama walivyofanya Mbeya City msimu wa kwanza?

Tano Bora ya misimu miwili…
2013/2014
                      P       W       D       L       F       A       GD       PTS      
1. Azam    26       18       8       0       51       15       36   62      
2. Yanga   26       16       8       2       61       19    42      56      
3. Mbeya   26      13       10    3       32       19     13        49      
4. Simba     26       9       11       6       41       27   14      38      
5. Ruvu      26       10       8     8   28       32       -4          38      


2012/2013      

                        P       W         D       L         F       A       GD       PTS      
1. Yanga       26       18       6       2       47       14       33       60      
2. Azam               26       16       6       4       46       20       26       54      
3. Simba       26       12       9       5       38       25       13       45      
4. Kagera       26       12       8       6       27       19       8       44      
5. Mtibwa       26       10       9       7       29       25       4       39      






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic