October 9, 2014



COASTAL UNION IKIPAMBANA NA SIMBA WAKATI IKITUMIA JEZI ZENYE UDHAMINI WA SOUND MSIMU ULIOPITA.

Makamu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mguto ameonyesha kubabaika kuhusiana na uamuzi wa klabu hiyo kutaka kuifungulia mashitaka kampuni ya Bin Slum Tyres Ltd.

Mguto amesema suala hilo lilijitokeza kwenye kikao chao cha kamati ya utendaji, lakini lilikuwa wazo la mjumbe mmoja tu.
MGUTO (KULIA) AKIWA NA MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA COASTAL UNION, SALIM AMIR.

Akihojiwa na Redio One jana, Mguto alionekana kubabaika baada ya kuulizwa kama aliona ni sahihi wao kufungua mashitaka.
“Kwa kweli naomba tuliache, maana ni suala ambalo lilikuwa ni wazo la mjumbe mmoja tu kwenye kikao.
“Nashindwa kusema sawa au la, lakini acha kwanza tusubiri,” alisema.
Alipoulizwa kuwa, kama sasa wanashinikiza mashabiki wa Coastal Union kutovaa jezi za zenye nembo ya mdhamini Sound, msimu ujao wakiachana na mdhamini wa sasa Pembe, watawazuia tena mashabiki kutovaa?
“Kwa kweli hapo una hoja ya msingi, ndiyo maana nakuambia tuliache kwanza suala hilo kwa sasa,” alisema Mguto.
Sakata hilo limezidi kupaa baada ya uongozi wa Coastal Union kushinikiza mashabiki wakamatwe na Polisi kwa kuingia uwanjani wakiwa na jezi hizo.
Lakini baadaye Polisi iliona hakuna kesi na kuifuta, baadaye Bin Slum aliyemwaga Sh milioni 300 akiwa mfadhiri wa timu hiyo akajitokeza na kupinga jambo hilo.
Hali iliyooonyesha kuudhi uongozi wa Coastal Union na kutangaza kufungua kesi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic