Ingawa haijazitendea haki kwa kupata mabao mengi zaidi, Barcelona ndiyo
timu inaongoza kwa kupata kona nyingi zaidi katika La Liga, msimu huu.
Chini ya Kocha Luis Enrique, Barcelona imeishapiga kona 67 ambazo ni
nyingi zaidi kuliko timu nyingine.
Inafuatiwa na Sevilla na Real Madrid, kila moja ina 50.
Timu nyingine zilizopiga kona nyingi ni Valencia iliyopiga kona 37,
Atlético (58) na Celta kona 55.
Shida na kinacholalamikiwa na mshabiki wake kuwa Barcelona inapata kona
nyingi lakini hazina manufaa kwa kuwa hawazitumii kupata mabao.
0 COMMENTS:
Post a Comment