October 20, 2014


Mshambuliaji wa Simba, Mkenya Paul Raphel Kiongera, amefunguka kuwa pamoja na wao kushindwa kuibuka kidedea dhidi ya Yanga, wachezaji wa timu yake walionyesha uwezo, hasa kipa kinda Peter Manyika aliyehimili mikikimikiki ya wapinzani wao.


Kiongera alikuwa jukwaani akiwa na mwanaye wanaishuhudia mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara.
Baadaye mshambuliaji huyo alisema alifuatilia mchezo huo kwa umakini na ilikuwa ni mara yake ya kwanza kushuhudia Simba na Yanga akiwa Tanzania, lakini aliridhishwa na kiwango cha wenzake ambao walicheza.
Alisema timu yake isikate tamaa, zaidi iendelee kujituma katika michezo ijayo kwa sababu walifanya kazi kubwa katika mchezo wa juzi, hasa kipa ambaye ilikuwa mechi yake ya kwanza ya ligi.
“Kiwango walichokionyesha Simba kilikuwa kizuri, walifanya kazi kubwa, japo walipoteza nafasi nyingi lakini Manyika amefanya kazi nzuri katika mchezo wa juzi, ingawa ulikuwa na ushindani mkubwa,” alisema Kiongera.


Kiongera kwa sasa anaendelea na matibabu, muda si mrefu anaweza akarejea uwanjani na kuungana na timu yake baada ya maendeleo yake kuwa mazuri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic