October 20, 2014


Katika hali isiyo ya kawaida, mashabiki wa Yanga walivaana na kushambuliana wenyewe kwa wenyewe, kisa kikiwa ni kuwasema vibaya wachezaji wawili wa timu hiyo, Mnyarwanda Haruna Niyonzima na Mbrazili Andrey Coutinho.

Hiyo ilijiri juzi kwenye majukwaa ya Uwanja wa Taifa jijini Dar, Yanga ilipokuwa inaumana na Simba na kutoka suluhu.

Sekeseke hilo lilianza kuunguruma baada ya shabiki mmoja wa timu hiyo kutoa kauli kuwa Niyonzima na Coutinho wanapenda mpira wa shoo na wanaigharimu timu, hivyo ni bora watolewe.

Kauli hiyo ilionekana kuwachefua mashabiki wengine waliokuwepo jukwaani hapo ambapo ghafla walimvaa kwa kumtupia maneno makali na kumtaka afute kauli yake hiyo mara moja la sivyo aondoke kwenye jukwaa, kitu ambacho shabiki huyo alikipinga.
Kutokana na mgomo huo, jukwaani hapo paliibuka mzozo mkubwa mpaka baadhi ya mashabiki wengine waliokuwa jirani na jukwaa hilo, walipoingilia na kuwaweka sawa mashabiki hao wakiwasihi kuwa wote ni kitu kimoja na haina haja ya kugombana.
Katika hatua nyingine, mashabiki wengine pia walisikika wakitupiana matusi baada ya shabiki mmoja kuropoka kuwa Mrisho Ngassa hakustahili kuanza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo siku hiyo bila ya kutoa sababu maalum.

Zogo ambalo lilizimwa baada ya mmoja wa mashabiki hao waliokuwa wakitukanana, kurudi chini na kuwa mpole.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic