October 23, 2014

MWAMWAJA.

Kocha Mkuu wa Prisons ya Mbeya, David Mwamwaja amesema hakutakuwa na kazi lahisi kwa Simba.
Prisons itakuwa mwenyeji wa Simba katika mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu Bara nje ya Dar es Salaam katika msimu huu.

Tayari Simba imecheza mechi nne na kutoka sare zote kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Mwamwaja aliyewahi kuinoa Simba amesema kazi itakuwa ngumu na Simba isitarejie mteremko hiyo wikiendi.
“Tumejiandaa kwa kuwa tunataka kurekebisha makosa ya kufungwa na JKT.
“Tulicheza vizuri katika mechi iliyopita, lakini si kwa kiwango cha juu sana. Sasa tunaweza kuitumia nafasi ya kurekebisha makosa dhidi ya Simba,” alisema Mwamwaja mmoja wa makocha wakongwe wazalendo.
Katika mechi yake ya mwisho, Simba iliyotua mjini Mbeya jana ilitoka sare dhidi ya Yanga wakati Prisons ilipoteza dhidi ya JKT Ruvu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic