October 22, 2014


Kiungo mchezeshaji wa Yanga Myarwanda, Haruna Niyonzima, ameamua kuvunja ukimya na kusema anasumbuliwa au hajaukamata vizuri mfumo wa kocha mpya, Marcio Maximo.

Niyonzima alishindwa kuonyesha kiwango cha juu katika mechi iliyopita, Yanga ilipowavaa watani wake Simba.

Niyonzima raia wa Rwanda amesema kuwa mfumo wa uchezaji anaoutumia kocha wake ndiyo umesababisha yeye acheze chini ya kiwango na siyo kitu kingine.

Niyonzima alisema, mfumo anaoutumia kocha wake huyo wa kufanya mashambulizi ya kushtukiza ‘Counter Attack’ yeye hauwezi tofauti na wachezaji wenzake.

Myarwanda huyo alisema, yeye hawezi kucheza mfumo huo, mwenyewe amezoea soka la pasi, akiamini ndiyo linalomfanya aonekane bora katika mechi zao za Ligi Kuu Bara na mashindano mengine.
“Mashabiki ujue walikuwa hawajanigundua, mimi kucheza chini ya kiwango siyo kwenye mechi dhidi ya Simba, mechi nyingi nimekuwa sionekani kutokana na mfumo anaoutumia kocha wetu.
“Kocha anataka tucheze mipira mirefu ya kushambulia kwa kushtukiza kwenye lango la timu pinzani, ambao kwangu ni mgumu, kiukweli siuwezi kabisa, mimi ninataka tucheze mpira wa pasi nyingi.
“Ninaamini tukiendelea kuutumia mfumo huo, basi nitaonekana kiwango kushuka kadiri ya siku zitakavyokwenda, ili nionekane bora tucheze soka la pasi lakini hivi nitapotea,”alisema Niyonzima ambaye amekuwa akianza michezo yote ya Yanga msimu huu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic