WAZIRI NKAMIA AKIWA OFISINI KWAKE... |
Na Saleh Ally
SERIKALI imeamua kuvunja ukimya kuhusiana na
suala la kuwaandaa vijana ambao watakuwa nyota wa taifa hapo baadaye.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana na Utamaduni,
Juma Nkamia amesema litakuwa ni jambo la msingi kama Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) litaangalia wakati huu kuwa mwafaka wa kuwapa nafasi vijana.
Nkamia amesema vijana wanapoandaliwa kwa
muda wa kutosha ni vizuri kwenda mbali wakiwa imara kwa kuwa msingi wao ni
bora.
AKIWA OFISINI KWAKE.... |
Vijana:
Katika mahojiano maalum na Championi
Jumamosi, ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Nkamia amesema wakati wa michuano
itakayofanyika Novemba nchini Ethiopia litakuwa ni jambo zuri kikosi
kitakachoundwa kwa timu ya Tanzania Bara kutoa nafasi kwa vijana wengi.
“Vijana kawaida wanakuwa tegemeo la baadaye,
lakini utaratibu ni lazima waandaliwe. Pamoja na mazoezi, vijana wanatakiwa
kupewa kitu kigumu kwao. Michuano ya Chalenji itakuwa ni sehemu sahihi.
“TFF ikae na kuzungumza na mwalimu wa timu
ya taifa, imueleze kwamba wanataka kuandaa vijana na wakongwe kama akina Kelvin
Yondani, Amri Kiemba na wenzao wapunguzwe kidogo.
BAADA YA MAHOJIANO NA SALEH ALLY... |
“Sisemi wote watoke, lakini nafasi ya vijana
iwe kubwa kwa kuwa wachezaji hao ndiyo wanaondoka hivyo. Sasa ni vizuri kuwapa
nafasi vijana ili kuwa na timu imara hapo baadaye,” anasema Nkamia na
kusisitiza.
“Tunaweza kufurahia sasa kushinda mechi za
kirafiki na kupata nafasi nzuri kwenye viwango vya Fifa, lakini haina faida
kubwa kama vijana wakiandaliwa, Tanzania ikawa na timu bora na imara halafu
ikaweza kufuzu kucheza Kombe la Mataifa hapo baadaye.”
DK NDUMBARO |
Dk
Ndumbaro:
Pamoja na hivyo, Nkamia ambaye kitaaluma ni
mwandishi, amelizungumzia suala la kufungiwa kwa mwanasheria maarufu nchini Dk
Damas Daniel Ndumbaro kama ni jambo linalishangaza na kusikitisha.
Nkamia ambaye ni Mbunge wa Kondoa Kusini
anasema TFF imekurupuka na kutumia jazba katika suala hilo na ilifanya maamuzi
baada ya serikali kuwa imeingilia na kuagiza TFF na klabu kukutana kupata
mwafaka.
“Sijui hata nitumie neno gani ili nieleweke
sahihi, nianze hivi; ninawaunga sana mkono TFF katika masuala ya maendeleo ya
mchezo wa mpira hapa nyumbani.
“Lakini serikali haitawaunga mkono hata
kidogo kwa kitendo kama hicho cha kumfungia Dk Ndumbaro. Kwanza wameonyesha
walifanya mambo kwa jazba, walikirupuka na walitaka kutekeleza hilo.
“Wazungu wanasema a good listener is a good
speaker (msikilizaji mzuri huwa msemaji mzuri). Hasira haziwezi kusaidia
maendeleo ya mchezo wa soka nchini.
“Tayari sisi (serikali) tuliishangilia,
tukawataka kukutana na baadaye kurejea kwetu. Kabla hata ya kukutana, wakafanya
wanayojua, wakamfungia Dk Ndumbaro kwa miaka saba.
“Nilimsisitiza Malinzi kwamba wanapaswa
kukaa na kulimaliza kwa mazungumzo, lakini ajabu haikuwa hivyo, sijui
alinipuuza nilichozungumza naye, naona akaitisha kamati, mambo yakaenda haraka
na Dk Ndumbaro akafungiwa.
“Miaka saba si kitu kidogo, adhabu hata
ingekuwa kuna kosa kweli ni kubwa sana. Hawawezi TFF kufanikiwa kwa kuwa
wanafungiana au kutisha watu hasa kwa wale wanaojaribu kurekebisha kunapokuwa
kuna kosa.
“Nimesikia wanasema Dk Ndumbaro
alimdhalilisha Rais wa TFF, wapi sasa! Kwani alikuwa anazungumza mwenyewe tu,
alifanya hivyo kwa niaba ya klabu, hilo liko wazi kwa kuwa klabu zilionyesha
kupinga hilo na utaratibu uliotumika. Maana yake wakati wanakaa, bado Dk
Ndumbaro angekuwa upande wa klabu.
“Kumfungia kunaashiria nini, labda
waliipuuza serikali! Kwanini wasingekaa na kumalizana, kuzungumza kunapokuwa na
tofauti ndiyo jambo zuri, si kupeana adhabu kama hizo au kutishana. TFF hawajui
tu, kufanya hivyo kunaweza kuwasababisha kukosa vitu vingine,” anasema Nkamia.
“Tuliwaambia baada ya bunge ambalo linaanza
Novemba 4, tutakutana. Sasa tusichekeshe watoto kwa kuonekana ni watu
tunaolumbana tu. Na itakuwa vizuri kwa TFF kurudi na kuiangalia hiyo adhabu kwa
kuwa haina faida kwenye soka hapa nyumbani.”
Kuhusianiana na serikali kama inaweza kuwa
na bajeti kwa ajili ya kusaidia soka la watoto na vijana, Nkamia anasema bado
hawana bajeti ya kutosha.
“Serikali ina mambo mengi sana, kuna wakati
inahitaji kusaidiwa mambo fulani. Lakini tunaamini tunafikia huko katika siku
za usoni, ni suala la kulifanyia kazi na tumekuwa tukilijadili kwa kuwa
tunapenda kuona vijana wanaendelezwa na ndiyo nguzo ya maendeleo yas michezo
nchini,” anasema Nkamia na kuongeza.
“Lakini tayari nimezungumza na BMT na
kuwataka kuandaa plani, kwamba tunaweza kufanya vipi katika kusaidia michezo na
hilo litasaidia katika siku za usoni.
“Pia unaweza kuandaliwa mfumo maalum ambao
utakuwa unachangiwa kwa njia mbalimbali lakini kwa makubaliano, si kulazimisha
watu. Mfano Kampuni ya Bia ya TBLna Bakheresa wanajitahidi kuchangia michezo,
hivyo tunawapongeza na tunaomba wengine pia wajitokeze.”
Serikali iliamua kuingilia suala hilo baada
ya klabu kupinga kukatwa asilimia 5 katika fedha zinazopata kutoka Vodacom na
Azam TV kwa ajili ya udhamini wa Ligi Kuu Bara.
Dk Ndumbaro ambaye pia ni Mhadhiri wa Vyuo
Vikuu vya Dar es Salaam (UDSM) na kile cha Huria (Out), akazungumza kwa niaba
ya klabu za ligi hiyo, zikipingwa kukatwa fedha hizo na mwisho kusababisha
serikali kusikia kilio cha klabu na kuliingilia suala hilo.
Serikali kupitia Waziri Nkamia ilifanikiwa
kuzima zoezi hilo kwa kuwa klabu tayari zimelipwa fedha zao za udhamini kupitia
Bodi ya Ligi Tanzania (TPL). Lakini ikasisitiza klabu na TFF kukutana.
Suala hilo ndiyo lilionyesha kuwaudhi TFF,
ambao walimfungulia mashitaka kwenye kamati ya nidhamu ambayo iko chini yake,
nayo ikatoa adhabu Dk Ndumbaro akiwa nje ya nchi ambako amepata mwaliko wa moja
ya vyuo vikuu vya nchini Marekani.
0 COMMENTS:
Post a Comment