October 25, 2014


Na Saleh Ally 
LUIS Suarez, leo hana ujanja na wala hawezi kukwepa kwamba anatakiwa kufanya kazi ya ziada au kitu kitakachoushitua ulimwengu kuonyesha sasa amerejea kwenye soka la ushindani.


Kifungo cha miezi minne kutokana na kumng’ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini kimepita. Pamoja na kuwaangalia nyota Cristiano Ronaldo na Lionel Messi watafanya nini leo kwenye mechi ya wapinzani wakubwa, Real Madrid dhidi ya Barcelona ‘El Clasico’, bado Suarez atatupiwa macho zaidi.

Wengi watamtupia macho Suarez ambaye atakuwa na madeni kibao huenda kuliko Ronaldo na Messi au Gareth Bale na Neymar.

Suarez aliingia kwenye ‘pea’ ya tatu ya El Clasico. Pea za klabu hizo mbili kongwe imejipanga hivi, ya kwanza ni Ronaldo na Messi, inafuatia Neymar na Bale, halafu James Rodríguez na Suarez.

Pea ya tatu inakutana kwenye mechi hiyo yenye rekodi zisizofutika na kila jambo linalofanyika kuanzia dakika ya kwanza hadi ya mwisho linaingia kwenye rekodi.

Deni namba 1:
Barcelona ilikubali kumtwaa Suarez katika kipindi cha matatizo, licha ya kuwa amefungiwa kwa kumng’ata Giorgio Chiellini wa Italia, ikamsajili hivyohivyo kwa dau kubwa la pauni milioni 72 (Sh bilioni 187).

Deni namba 2
Barcelona walijiua Suarez amekosea, lakini wakafumba macho na kuanza kumtetea kupita kiasi utafikiri alisingiziwa au wakati Chiellini anang’atwa, Suarez hakuwepo!

Deni namba 3:
Ili acheze, lazima mchezaji mmoja akae benchi, mfano Pedro Rodriguez. Kama akianzia benchi lazima mchezaji huyo acheze, hivyo akiingia lazima aonyeshe kweli walikuwa sahihi kumuingiza.

Deni namba 4:
Mashabiki wa Barcelona nao ‘walijiwehusha’ kama uongozi wao, wakamuunga mkono kupita kiasi, hivyo leo wataona faraja kubwa akifunga bao ambalo litakuwa ni la kuwamaliza au kuchangia kuishinda Madrid kwao Bernabeu.

Deni namba 5:
Barcelona imemchukua kwa kuwa msimu uliopita ndiye alikuwa mfungaji bora England na Ulaya baada ya kufunga mabao 31.

Vipi atashindwa kufunga hata moja leo? Barcelona inataka kuweka rekodi nzuri kwa kuwa tangu ianze kukutana na Madrid, Mei 3, 1902 imefunga mabao 364 wakati wenyeji wake hao wa leo wana mabao 384.

Anaweza kuwa na madeni lukuki katika siku yake ya kwanza kuichezea Barcelona kwa kuwa ni kikosi kikubwa. Lakini ushindi dhidi ya Madrid wakiwa nyumbani, ndiyo deni kuu ambalo mashabiki wa Barca wanataka kuona likilipwa. Suarez ni mtukutu na ana uwezo mkubwa, bila ya kujali ataingia au kuanza, bado ana nafasi ya kufanya vema.

TAKWIMU:
Real Madrid
Ushindi        91
Sare                 48

Barcelona
Ushindi       88

Real Madrid - mabao        384
Barcelona - mabao            368
Jumla ya mechi               227

Takwimu za nyumbani:
                      Ushindi    Sare     Kupoteza
Madrid                            65      25            25     
Barcelona                 63      23            26



SUAREZ, MZEE WA MAJANGA
Juni 2014 - Alimuuma Giorgio Chiellini (akafungiwa miezi minne).

Aprili 2013 – Alimuuma Branislav Ivanovic (Akafungiwa mechi 10).

Des. 2011 – Alitoa ishara mbaya kwa mashabiki Fulham (akafungiwa mechi 1).

Des. 2011 – Alimbagua Patrice Evra (Akafungiwa mechi 8).

Nov. 2010 – Alimuuma Otman Bakkal (Akafungiwa mechi 7).

Julai 2010 –Alilambwa kadi nyekundu mechi dhidi ya Ghana, kwa kushika makusudi katika Kombe la Dunia.

Nov. 2007 – Alizozana na wachezaji wenzake (Ajax ikamsimamisha).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic