November 2, 2014


Mwanasheria maarufu nchini, Dk Damas Ndumbaro ameendelea kumuumbua Rais wa TFF, Jamal Malinzi baada ya kuonyesha asivyo makini kwa mara nyingine.

Dk Ndumbaro ameonyesha uthibitisho wa kupokelewa kwa rufaa yake ambayo siku moja tu Malinzi alisema Dk Ndumbaro hakuwa amewasilisha rufaa yake ya kupinga kufundiwa miaka saba.
Katika ‘document’ hiyo inaonekana imesainiwa na mmoja wa maofisa wa TFF na ilipokelewa tokea Oktoba 21.
“Sasa unaona kama Malinzi hajui hii document imepokelewa ofisini kwake.
“Tena kabla ya kuuliza anakwenda kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari. Hii ni sehemu ya kuonyesha si makini.
“Kesi yangu ilisikilizwa ndani ya siku nne, lakini leo ni zaidi ya wiki, rufaa yangu haijasikilizwa na nimeishalipa TFF shilingi milioni moja ya rufaa.

“Haya yote yamefanyika ofisini kwa Malinzi lakini yeye halijui hilo,” alisema Dk Ndumbaro akionyesha kujiamini.

2 COMMENTS:

  1. Tatizo lako saleh ni elimu duni na ufahamu wa sheria uliokuwa nao.
    Hapo hakuna rufaa iliyokatwa kisheria hiyo document inaonyesha kusudio la rufaa na vipengele vya hiyo rufaa na si rufaa kisheria.Poor you!

    ReplyDelete
  2. Kweli nimegundua watanzania wengi hasa hawa wakamata kalamu ni mambumbumbu wa sheria na hata kimalkia kimewapita njiani!
    Yaani Memorandum of Appeal mtu anaandika na kukomalia eti Ngumbaro kakata rufaa,aibu iliyoje?!
    Saleh Ally unatuaibisha ndugu zako!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic