KISIGA AKIITUMIKIA SIMBA. |
Wachezaji watatu wa Simba ambao walisimamisha
na kamati ya utendaji wa utovu wa nidhamu na kucheza chini ya kiwango, jana
hawakutokea kwenye kikao kilichotakiwa kuwakutanisha na viongozi wao.
Kikao hicho kilikuwa maalum kwa ajili ya
viongozi kuwasikiliza na kutaka kujua nini kilitokea, kama wana makosa au la!
Baada ya hapo, uongozi ungekuwa na nafasi ya
kutafakari na kuona makosa yalipo, halafu wahusika wangeadhibiwa au vinginevyo.
CHANONGO |
Wachezaji Amri Kiemba, Shabani Kisiga na
Haruna Chanongo, wote hawakutokea katika kikao hicho.
Kisiga pekee, ndiye alipiga simu kutoa udhuru
tena baada ya muda waliotakiwa kufika kwenye kikao kuwa umepita.
Awali niliandika makala, nikiwashauri viongozi
wa Simba kutenda haki kwenye kikao hicho na kuwa makini wakiachana na hisia,
badala yake waangalie usahihi kabla ya kufikia kuhukumu.
Lakini leo, nasema wazi nimeshangazwa sana na
uamuzi huo wa akina Kisiga, Kiemba na Chanongo kuacha viongozi wao akiwemo Rais
wa Simba, Evans Aveva anakwenda sehemu, anawasuburi, hawatokei halafu wanakaa
kimya.
Ni picha mbaya sana, hali inayoweza kujenga
hata hisia zisizo sahihi. Pili inaonyesha kweli wao ni watovu wa nidhamu.
KIEMBA |
Hakuna ambacho wanaweza kujitetea zaidi ya
kuomba radhi. Huenda mwanzo hakukuwa na tatizo kwao na ingejulikana baada ya
kukutana na uongozi wao.
Lakini sasa kuna tatizo, tena liko wazi kwamba
wameonyesha utovu wa nidhamu. Hata Kisiga anaweza kuwa na nafuu, lakini
alikosea.
Kiemba aliwahi kusema kama riziki imeisha Simba,
basi! Sahihi, riziki hutoa Mwenyezi Mungu, lakini hata mara moja hajawahi kutoa
utovu wa nidhamu.
Hivyo Kiemba alipaswa kwenda kwenye mkutano,
alitakiwa kuzungumza bila ya woga na mwisho aache uamuzi utaotolewa. Kama
angeonewa, basi kweli riziki ndiyo imeisha na Mungu angempatia nyingine.
Lakini kitendo cha kumuweka kiongozi mkubwa wa
klabu ambaye amejitokeza kwenda kukusikiliza, sasa kunakuwa hakuna tena lawama
kwake badala yake ni wachezaji.
Lengo la SALEHJEMBE si kutetea upande wowote,
haki itendeke ndiyo muhimu zaidi.
Lakini msisitizo, kwa walichofanya Kiemba,
Kisiga na Chanongo ambaye ni chipukizi, si kitendo sahihi na wanapaswa
kujitathmini upya kwa kuwa katika dunia hii, hakuna aliyewahi kufanikiwa kwa
ubora wa kiburi chake.
Uki sahihi sana wakitakiwa wajajibu tuhuma kwa kuwa walikuwa hawajadhibiwa bado. Kibongo bongo usikute kuna watu washawapa kichwa waachane na simba watawasajili
ReplyDelete