November 2, 2014


Kocha Msaidizi wa Kagera Sugar, Mlage Kabange amejivunia ubora wa bao lililofungwa na mshambuliaji wake Paul Ngwai katika mechi dhidi ya Yanga.

Yanga ililala kwa bao 1-0 katika mechi hiyo dhidi ya Kagera ikiwa nyumbani Kaitaba mjini Bukoba, jana.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Kabange alisema bao alilofunga Ngwai linawafanya Yanga wasiwe na cha kulalama.
Ngwai alifunga bao hilo ukiwa ndiyo mpira wake wa kwanza anaugusa baada ya kuingia. Krosi ya juu ambayo aliunganisha moja kwa moja na kumuacha Deo Munishi 'Dida' akiduwaa.

“Ni bao bora kabisa ambalo halina ubishi, bao kama yale ambayo unaweza kuyaona Ulaya.
“Hilo litakuwa moja ya mabao bora kabisa na utakubaliana na mimi kama uliliona,” alisema kocha huyo.
“Kwa kweli tiliyafanyia kazi makosa ya mechi zilizopita, halafu tukawa tayari kwa ajili ya Yanga na kweli umeona soka letu.

“Yanga walicheza vizuri, huenda hawakuwa pia na bahati lakini hii ilikuwa siku yetu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic