November 2, 2014


Wakati Kocha Msaidizi, Leonardo Leiva alilambwa kadi nyekundu katika mechi ya Yanga dhidi ya Kagera, bosi wake amesema wachezaji wa timu hiyo ya Bukoba waliharibu mchezo kwa kupoteza muda.

Marcio Maximo amesema Kagera walipoteza muda makusudi katika mechi yao ya Ligii Kuu Bara kwenye Uwanja wa Kaitaba, jana.
“Walipoteza sana muda, mwamuzi ameona hiyo hali lakini ajabu kaongeza dakika tatu tu.
“Haikuwa sahihi na hii si haki hata kidogo. Imenishangaza sana, nafikiri mnafurahia kuona Yanga inapoteza,” alisema Maximo.

Yanga ililala kwa bao 1-0 katika mechi hiyo dhidi ya Kagera ikiwa nyumbani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic