November 7, 2014


Uongozi wa Mbeya City umesema kupoteza mechi tatu mfululizo haliwezi kuwa jambo litakalowavuruga.

Badala yake, Mbeya City wamesisitiza watakuwa wakifanya mambo yao kutatua matatizo.
Msemaji wa Mbeya City, Dismas Ten amesema tayari Kocha Juma Mwambusi amekuwa akifanya marekebisho kabla ya mechi dhidi ya Stand United mjini Shinyanga.
“Tayari tuko Shinyanga, jana tulicheza mechi ya kirafiki na leo kocha amekuwa akimalizia maandalizi.
“Kupoteza hakuwezi kutufanya tuanze kulumbana na kulaumiana. Tumemuachia kocha afanye anachoona ni sahihi.

“Bado tunaamini tutarudi katika njia sahihi na kuendelea kupambana,” alisema Dismas Ten.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic