November 7, 2014


Msemaji wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru haishi maneno lukuki, safari ameibuka na jipya.
Amesema kuwa kikosi cha Mtibwa Sugar hakitapoteza mechi yoyote.

“Mechi yetu inayofuata ni dhidi ya Kagera Sugar ndugu yangu. Itakuwa ngumu kwa kuwa hawa ndugu zetu kutoka Akagera ni wagumu na wana uwezo mzuri.
“Lakini ninachokuambia Mtibwa Sugar haitapoteza mchezo msimu huu. Kazi yetu ni kutoa vipigo hadi mwisho,” alisema.
“Lengo ni kuwa mabingwa na tutakuwa mabingwa, tulia uone.”
Hadi sasa katika mechi sita, Mtibwa Sugar haijapoteza hata moja baada ya kushinda nne na kutoka sare mbili.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic