December 8, 2014


Klabu ya Polisi Moro imeingia mkataba wa mwaka mmoja na aliyekuwa kiungo wa Simba, Zahoro Pazi.


Kiungo huyo aliwahi kukipiga katika klabu za   Mtibwa Sugar na Simba sasa ataanza kuonekana na kikosi cha Polisi.

Msemaji wa Polisi Moro, Clement Bazo, alisema kuwa wameamua kumsajili kiungo huyo kutokana na uwezo wake na wanaamini kuwa atawasaidia kwa kiasi kikubwa.

 Bazo alisema kuwa kwa sasa kikosi chao kinaendelea na mazoezi na wachezaji wanaoachwa katika kikosi hicho watatangazwa hivi karibuni.

“Tumemsajili Kiungo Zahoro Pazi  ambaye aliwahi kuitumikia Simba msimu uliopita, tunaamini uwezo wake na  umahiri alionao utaweza kuisaidia timu yetu kwa kiasi kikubwa msimu huu kwa sababu lengo ni kufanya vizuri.

“Na kama inavyofahamika ushindani umekuwa mkubwa sana, kila timu inajitahidi kuonyesha na kuhakikisha inafanya vyema na ili kuwa na kikosi bora kuna wachezaji takribani watano lazima watapigwa panga ili kuboresha kikosi,” alisema Bazo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic