December 8, 2014

SEHEMU YA ENEO LA HOTELI WATAKAPOWEKA KAMBI YANGA.
Bosi wa benchi la ufundi la Yanga, Marcio Maximo,  amesema ana uhakika wiki moja itamtosha kabisa kufanya kweli dhidi ya watani wao, Simba ambapo timu hizo zitakutana Jumamosi wiki hii kwenye mchezo wa Bonanza la Nani Mtani Jembe.


Yanga wanatarajia kuingia kambini leo Land Mark Bahari Beach kujiwinda na mchezo huo ambao watakuwa wakihitaji kulipa kisasi kufuatia mwaka jana kukubali kichapo cha mabao 3-1.

Maximo alisema kuwa kikosi chake kimejipanga vema ambapo anaamini kambi ya wiki moja inawatosha kabisa kujiweka fiti zaidi dhidi ya Simba.

“Tuna muda mfupi kabla ya mchezo ambao naweza kusema ni mgumu lakini naamini wiki moja inatosha kabisa kujiweka sawa zaidi kwa ajili ya mchezo huo,” alisema Mbrazili huyo.

Kichapo cha Yanga mwaka jana kilisababisha kuvunjwa kwa benchi zima la ufundi lililokuwa likiongozwa na Mholanzi, Ernie Brandts na Fred Felix Minziro.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic