December 31, 2014


Baada ya kucheza mchezo mmoja wa Ligi Kuu Bara chini ya Kocha, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, kiungo mchezeshaji wa Yanga, Haruna Niyonzima, ameibuka na kusema anaufurahia mfumo wa kocha huyo kwa kuwa unaifanya timu kucheza kwa kushambulia zaidi.


Kiungo huyo raia wa Rwanda alisema kuwa kocha aliyepita Mbrazil, Marcio Maximo alikuwa anataka zaidi soka la kushambulia kwa kushtukiza, lakini Pluijm anasistiza soka la pasi fupi, kasi na kushambulia muda wote, kitu ambacho ni kizuri kwani kinawapa presha wapinzani.

Niyonzima aliongeza kuwa yeye ‘ameupata’ haraka mfumo wa kocha huyo kwa sababu si mgeni katika kikosi cha Yanga, pia ndiyo aina ya mfumo unaomfanya acheze ‘atakate’ kwa sababu anapenda soka la kushambulia zaidi.

“Kukopi mfumo kwa haraka ni ngumu, lakini mwalimu huyu (Pluijm) si mgeni sana kwetu, labda baadhi ya wachezaji wachache ambao hawakuwepo awali akifundisha Yanga.

“Mfumo wake ni mzuri unatufanya tucheze pasi na kushambulia kwa haraka tofauti na Maximo ambapo tulikuwa tukitumia zaidi ‘kaunta ataki’ na kukaba sana ili wapinzani wasipate nafasi.

“Mfumo wa kushambulia ni mzuri zaidi kwa sababu lengo la timu ni kuchukua pointi tatu, sasa unaposhambulia muda mwingi unawapa presha wapinzani na kufanikiwa kupata unachokitaka,” alisema Niyonzima ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic