Klabu
ya Mtibwa Sugar inatarajiwa kuondoka siku ya Jumanne kuelekea jijini Mbeya
wilayani Kyela ambapo huko watacheza michezo ya kirafiki na timu za Super Ligi
za nchini Malawi ambapo TFF imetoa baraka katika hilo baada ya kupata mwaliko
kutoka Chama cha Soka Wilaya ya Kyela.
Mtibwa
mpaka sasa inashikilia nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi kuu ikiwa na
pointi 15 na kwa sasa timu zipo katika maandalizi kuelekea ligi kuu.
Ofisa
habari wa timu hiyo, Thobias Kifaru alisema kuwa wakiwa huko wataendelea na
mazoezi na kucheza michezo ya kirafiki na timu tofauti za Ligi Kuu ya Malawi kisha
watakwenda Songea mkoani Ruvuma.
“Lengo
kuu ni kuhakikisha kuwa tunajenga na kuimarisha kikosi chetu kuwa na ushindani
zaidi pindi ligi itakapoendelea ili kuweza kuwa katika nafasi nzuri ligi
inapokuwa inamalizika,” alisema Kifaru.








0 COMMENTS:
Post a Comment