December 6, 2014


Mshambuliaji mpya wa Simba, Mganda Dan Sserunkuma, anatarajiwa kutua nchini kesho Jumapili na kujumuika na wenzake Jumatatu ijayo kwa ajili ya kuendelea na programu za mazoezi ya timu hiyo.


Sserunkuma aliyesajiliwa na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Gor Mahia inayoshiriki Ligi Kuu ya Kenya, aliondoka nchini hivi karibuni na kurejea nyumbani kwao mara tu baada ya kumalizana na klabu yake mpya ambapo alienda kuchukua vifaa vyake.

Katibu wa Simba, Stephene Ally, alisema mchezaji huyo anatarajia kutua nchini kesho kabla ya kuungana na wenzake mazoezini siku ya Jumatatu (keshokutwa).

“Sserunkuma alienda kwao Uganda na tunatarajia atatua nchini Jumapili (kesho) hii tayari kwa kuanza kazi na klabu yake mpya ambapo atakuwa mazoezini siku inayofuata lakini bado hatujafahamu atakuja na ndege gani,” alisema Ally.


Simba kwa sasa inajiandaa na mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga itakayopigwa Jumamosi ijayo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic