December 6, 2014


Kiungo mkabaji wa Simba, Jonas Mkude amepewa mapumziko ya siku tatu kutokana na kusumbuliwa na Ugonjwa wa Malaria uliomuanza juzi Alhamisi.

Mkude alikumbwa na ugonjwa huo wakati akiwa kambini na wenzake kwenye kikosi hicho kilichopo kambini katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa ‘JKT’ maeneo ya Mbweni nje kidogo ya Jiji la Dar.

Simba inatarajiwa kuvaana na Yanga kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Yanga itakayopigwa Desemba 13, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe alisema kuwa kwa sasa Mkude anaendelea vizuri na wanatarajia atarudi kwenye hali yake baada ya siku tatu.

“Mkude anaendelea vizuri baada ya jana (juzi) kupimwa na kukutwa ana wadudu wawili wa malaria na tunatarajia kwa muda wa siku tatu tuliompa ili apumzike atakuwa fiti na kujiunga na wenzake kuendelea na mazoezi,” alisema Gembe.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic