January 7, 2015


Kiungo wa West Ham, Alex Song amestaafu kuichezea timu yake ya taifa ya Cameroon.

Song amestaafu na kutundika kwenye mtandao kwamba ameamua kutoichezea Cameroon kabisa.


Hali hiyo imeamsha furaha kwa Kocha wa West Ham, Sam Allardyce ambaye anasikia faraja kubwa kuendelea kumtumia kwenye Ligi Kuu England.

Hata hivyo, Allardyce amekuwa makini ushiriki wake katika jambo hilo akihofia Fifa kuona amemshinikiza.

Song anaonekana kuwa na hasira ya kuachwa kwenye Kombe la Mataifa Afrika lakini pia mfarakano na kocha wake ambaye alimtaka kuomba radhi baada ya kupiga kiwiko kwenye Kombe la Dunia nchini Brazil.


Lakini Song hakufanya hivyo, mwisho akaamua kumtema hali iliyozua utata huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic