January 16, 2015


Baada ya matukio mbalimbali ya waamuzi kupigwa katika viwanja tofauti katika mechi za Ligi Daraja la Kwanza, Chama cha Waamuzi wa Soka Tanzania (Frat), kimelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwawekea bima waamuzi.


Akizungumza kwa uchungu kutoka mkoani Shinyanga, Mwenyekiti wa Frat, Mwalimu Nassoro, alisema inasikitisha kuona waamuzi wanapigwa kutokana na sababu ambazo hazieleweki huku akiwataka TFF kuwa na sheria kali pamoja na kuwawekea bima waamuzi.

“Nimeshangaa sana matukio hayo, ajabu hata askari ambao wanatakiwa kulinda amani nao ndiyo wanageuka kuwa wa kuwapiga waamuzi, wanataka waamuzi tukimbilie wapi?” alihoji kiongozi huyo.

Aliongeza kuwa, Frat inalaani matukio hayo yakiwemo ya timu za Polisi Dodoma na Polisi Mara kuwashambulia waamuzi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic