January 16, 2015


Kitendo cha kipa wa Simba, Peter Manyika kutolewa katika dakika za mwisho kisha nafasi yake kuchukuliwa na Ivo Mapunda wakati wa fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya Mtibwa Sugar, kimezungumzwa na mzazi wa chipukizi huyo, Manyika Peter.


Baba mzazi wa kipa huyo, amesema kuwa mwanaye ilikuwa lazima atolewe kwa kuwa kiwango chake kimeshuka katika siku za hivi karibuni, ndiyo maana akatolewa dakika chache kabla ya mechi kuamuliwa kwa matuta.


Katika mechi hiyo, Simba ilitwaa ubingwa kwa penalti 4-3 huku Mapunda akiibuka shujaa baada ya kupangua mkwaju wa mwisho uliopigwa na Vincent Barnabas.

“Ilikuwa afadhari Manyika kutodaka penalti kwa sababu kiwango chake hakikuwa kizuri, kwa ninavyomfahamu naona ameshuka kiwango tofauti na alipokwenda Simba mara ya kwanza.

“Nafikiri sasa ana nafasi ya kurejesha kiwango chake kupitia mazoezi,” alisema Manyika.

Manyika ni kati ya makipa makinda nchini ambao wanafanya vema na ameitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars Maboresho.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic